Tuesday, June 4, 2013

Vifaa vipya vya Manuel Pellegrini

KIUNGO Jesus Navas amesema anafurahia kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na kocha mpya wa Manchester City, Manuel Pellegrini.
Navas anatua Etihad kwa dau la Pauni Milioni 23 kutoka Sevilla huku kocha wa Malaga, Pellegrini anajiandaa kuthibitishwa kurithi mikoba ya Roberto Mancini.
Winga huyo wa kulia, ambaye amekuwa akichezea tangu anaibuka hadi sasa, anaamini uhamisho huo utakuwa wa mafanikio kwa wote, klabu na mchezaji.
First foot forward: Jesus Navas (left) has said he is delighted to have joined Manchester City from Sevilla
Jesus Navas (kushoto) anafurahia kujiunga na Manchester City kutoka Sevilla
New boss: Manuel Pellegrini is set to be confirmed as manager at the Etihad after Roberto Mancini's sacking
Kocha mpya: Manuel Pellegrini anajiandaa kuthibitishwa kocha mpya Etihad baada ya kufukuzwa kwa Roberto Mancini

"Nina furaha kujiunga na Manchester City. Ni nafasi nzuri kwangu na ninafikiri pande zote zina furaha. Niliamua kujiunga na City miezi minne iliyopita. Bado sijazungumza na Manuel Pellegrini, lakini ni kocha ninayemfahamu,".
Navas, aliichezea Hispania katika Fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2010, amesema hafahamu kama nyota mwenzake wa La Liga, Isco, anayechezea timu ya Pellegrini, Malaga naye anakuja City.
National star: Navas will meet up with the Spain squad for the Confederations Cup this summer
Nyota wa taifa: Navas ameitwa kwenye kikosi cha Kombe la Mabara cha Hispania

"Sijui kama Isco atakuja pia. Tutaona. Ligi Kuu ni ya kasi sana na ninavutiwa nayo, kwa sababu Manchester City wametengeneza timu nzuri pamoja. Naondoka Sevilla, ambayo ni sehemu nzuri na ninakwenda katika klabu kubwa England. Bado siwezi kuzungumza Kiingereza vizuri. Nitajifunza sasa.
Thiago Alcantara
Isco
Wengine wanaokuja? Thiago Alcantara wa Barca (kushoto) na kiungo wa Malaga, Isco pia wanatakiwa Man City

Isco, pamoja na nyota wa Shakhtar Donetsk, Fernandinho, kiungo wa Barcelona, Thiago Alcantara, ni baadhi ya wachezaji wa mwanzoni ambao Pellegrini amewatambulisha wakati City inapigania saini zao hivi sasa kujenga kikosi cha kurejesha ubingwa wa Ligi Kuu England, walioupoteza kwa mahasimu wao, Manchester United.
Navas ameichezea mechi 23 nchi yake na atakuwamo katika kikosi mcha Vincente Del Bosque kitakachoshiriki Kombe la Mabara baadaye mwezi huu.

No comments:

Post a Comment