Sunday, May 26, 2013

FALCAO ATUA MONACO KWA EURO MILIONI 60

MSHAMBULIAJI Radamel Falcao anajiandaa kwenda kufanyiwa vipimo Monaco kesho kabla ya kujiunga na klabu hiyo ya Ligue 1, Ufaransa kwa dau la Euro Milioni 60, (sawa na Pauni Milioni 51,295,000, kwa mujibu wa taarifa nchini Hispania.
Mshambuliaji huyo wa Colombia kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa na kuihama Atletico Madrid kwenda Manchester United na Chelsea.
Pamoja na hayo, imetokea kwamba Monaco imepiga kasi na kuzipiku klabu zote na klabu hiyo iliyorejea Ligi Kuu Ufaransa pia inataka kuwasajili nyota wawili wa Porto, Joao Moutinho na James Rodriguez ambao kwa pamoja watagharimu kiasi cha Pauni Milioni 60.
Closing in: Highly-rated forward Radamel Falcao is on the verge of a big-money move to Monaco
Ameota mbawa England: Mshambuliaji wa gharama kubwa, Radamel Falcao yuko mbioni kutua Monaco
Got away: Falcao has been one of the most prolific players in Europe and was chased by Chelsea for a long time
Andondoka: Falcao amekuwa mmoja wa washambuliaji maarufu Ulaya na alikuwa akiwaniwa na Chelsea kwa muda mrefu
Prolific: The Columbian's goals helped his team Atletico Madrid on their way to winning the Spanish Cup
Kifaa: Mabao ya Mcolumbia huyo yameisaidia Atletico Madrid kutwaa Kombe la Hispania

Rais, Dmitry Rybolovlev ana hamu sana na kuwanyakua wachezaji wawili wa Porto, ambao ni wachezaji wenzake wa zamani Falcao aliyefunga mabao 32 katika mechi 36 msimu huu.
Kocha wa Atletico, Diego Simeone tayari amesema mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 hataacha pengo akiondoka na mchezo wa leo usiku wa La Liga dhidi ya Real Mallorca kwenye Uwanja wa Vicente Calderon unaonekana utakuwa wa mwisho kwake Rojiblancos.
Kocha Msaidizi wa Monaco, Jean Petit ameripotiwa kuiambia Radio RCN jana: "Ndiyo, tunamtarajia Falcao na wachezaji wengine wanne au watano wa kiwango chao,"alisema.

No comments:

Post a Comment