Tuesday, May 14, 2013

MPIRA NA MAENDELEO UPANGA MAGHARIBI JUMAMOSI USHINDI LAZIMA

Akizungumza kwa kujiamini asilimia zote unazozijua chini ya jua,katibu mkuu wa tawi la simba mpira na maendeleo kata ya upanga magharibi bwana NGUMI JIWE amesema kuwa katika kuelekea mtanange wa watani wa jadi jumamosi ya tarehe 18 mwezi huu wa tano lazima kualalumpa aka yebo yebo aka gongo wazi aka mwembe wa uani aka togwa la ngomani akamaiti yake kaburi aka TANO BILA lazima watachezea kichapo toka kwa MNYAMA SHABABI tena mchana kweupe maana walichokua wakitambia tayari kimedhibitiwa na ushindi lazima siku ya tukio.
 NGUMI JIWE ambaye wanachama wake siku zote wamezoea kumita mpambanaji amewataka viongozi wa juu wa simba kulitembelea tawi hili liloko maeneo ya faya jijini dar es salaam amesema kuwa kwa kufanya hivyo kutazidisha hamasa na kuweka wazi kuwa pamoja na uongozi wa juu kufanya mapambano lakini pia matawi kwa upande wao wananafasi ya kushiriki vizuri na kufanikisha NDALA kubeba taji huku akiugulia kichapo.

mwisho kabisa NGUMI JIWE alimaliza kwa kauli mbiu ya tawi hilo kwa kusema SIMBA NGUVU MOJA,
SIMBA TANO BILA NA HAZIRUDI.

No comments:

Post a Comment