
Tiketi kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Yanga litakalochezwa keshokutwa (Jumamosi) kwenye Uwanja wa Taifa zitaanza kuuzwa kesho (Ijumaa) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Vituo vitakavyouza tiketi hizo
kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers
ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom
Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live
Mbagala na Sokoni Kariakoo.
No comments:
Post a Comment