Tuesday, May 14, 2013

UONGOZI SIMBA WAKOSA IMANI NA MABADILIKO YA REFA ATAKAE CHEZESHA MECHI YAO NA MAFURIKO FC aka yanga


UONGOZI wa Simba SC umesema hauna imani na mabadiliko ya refa yaliyofanywa kuelekea mpambano wao na Yanga SC Jumamosi na kwa sababu hiyo unakutana katika kikao cha dharula haraka iwezekanavyo kujadili suala hilo, ikibidi kususia mchezo huo. Akizungumza na MPIRA NA MAENDELEO jioni hii, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba inayosimamia ushiriki wa timu katika mashindano pia, Zacharia Hans Poppe amesema kwamba uongozi utakutana haraka kujadili mabadiliko hayo. Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), amesema taarifa rasmi waliyokuwa nayo awali refa aliyepangwa kuchezesha mechi hiyo ni Israel Nkongo, lakini ajabu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) leo limemtaja refa tofauti, Martin Saanya.
  “Haiwezekani mabadiliko yafanyike ghafla, lazima kutakuwa kuna namna hapa. Tunakutana mara moja kujadili na kuchukua hatua, ikiwezekana tunaweza kugomea hiyo mechi, iwapo tutagundua kuna mchezo mchafu umeandaliwa dhidi yetu,”alisema Hans Poppe. Saanya kutoka Morogoro ndiye ameteuliwa kuchezesha pambano la watani wa jadi, Simba na Yanga SC la kufunga pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika mchezo huo, unaosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka nchini ili kujionea nani zaidi baina ya miamba hiyo, Saanya atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, wakati refa akiba atakuwa ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamisaa wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi atakuwa ni Leslie Liunda wa Dar es Salaam.
Taarifa nyingine zinasema mwamuzi huyo amebadilishwa kutokana na kuwa na taarifa za ‘mchezo mchafu’ ambazo yeye alizishitukia na kukataa kupokea fedha kwa ajili ya kuibeba timu moja.

No comments:

Post a Comment